FILAMU ZETU

KUFANANA KWA FILAMU BONGO NANI ALAUMIWE
 NB: Mada hii imejadiliwa na wapenzi wa filamu katika ukurasa 
          wa facebook....monalisafilms. maoni hayo si kutoka blog hii
          moja kwa moja. 

         Soko la filamu bongo linazidi kutanuka kila kukicha japo bado zinahitajika hatua nyingi mbele kufikia viwango vya kimataifa kama ilivyo kwa nchi za naijeria,Ghana na hata jirani zetu wa Kenya.
    Tanzania ikiwa imejikita katika tasnia ya filamu tangu mwanzoni mwa mwaka 2000 hadi sasa ni zaidi ya filamu 500 tofautitofuti zimekwishayafikia macho ya wapenzi wa filamu,kila mlaji (mnunuzi) wa filamu amekuwa akivutiwa na muigizaji wake ama mudhui ya filamu Fulani,mfano wapo wanaovutiwa na sinema za kivita,wengine mapenzi na wengine vichekesho.
Je wasanii wetu wanakidhi haja ya mlaji wao?? Hilo ndilo swali lililozuka na kuzua hii mada. Wachangiaji wakuu wakiwa ni wafuatiliaji wa filamu za hapa kwetu.
Majibu yalikuw tofautitofauti lakini malalamiko makubwa yalikuwa kwamba filamu nyingi za sasa katika soko zinjirudiarudia ama ni za kuiga kutoka nchi za wenzetu na kubadili lugha tu….na hapo ndipo swali la pili ambalo linaiendesha hii mada likiibuka,kwamba nani alaumiwe kwa hizi filamu kujirudia rudia???


 "SAADIZM"
UFINYU WA MAWAZO YA WATUNZI: Watunzi wengi kwa sasa wanakosa ubunifu,mtunzi akiwa dereva mkuu wa filamu inayokufikia nyumbani kwako anakuwa mvivu wa kutunga kitu cha kipekee na badala yake anaiga kutoka nje stori ileile na kuibadilisha lugha kisha kwa ujasiri anaifikisha kwa mtanzania kama filamu mpya.


 "KALUONA KINAWILO"
ELIMU YA SANAA:Waandaaji,wasimamizi na hata waigizaji wana kiwango kidogo cha elimu ya sanaa,wengi wao wamevamia fani kwa malengo tofauti hasahasa kutafuta umaarufu mtaani jambo hili linawalazimu kuchukua muda mrefu kupitia filamu za watu na kuchota kidogo kidogo ili na wao wafanye filamu hii inaturudisha katika giza ambalo tulikuwa tunaliacha.


"MICHAEL MSOMBE"
MIKATABA MIGUMU: kuna baadhi ya wasambazaji wana masharti magumu kwa wateja wao,utakuta mwandaaji amemsainisha mkataba mteja wake (msanii) unaomtaka kutoa filamu moja hadi mbili kwa mwezi yaani kwa mwaka filamu 24 za msanii mmoja ziingie sokoni,hapa kitatokea nini kama si kujirudiarudia kwa ujumbe kasoro wahusika?? Kwa hali halisi haiwezekani kichwa kimoja kitunge filamu 24 zote zikiwa na utofauti.
 "JOEL RENATUS"
MWANDISHI WA SCRIPT: Mazoea ya kumtumia mwandishi mmoja wa script katika filamu sio tu kwamba inadidimiza ama kuu vipaji vya waandishi wengine ila ni chanzo pia cha filamu kuwa na ujumbe unaofanana,mfano halisi ni katika utunzi wa vitabu vya simulizi,ladha ya kitabu cha Beka Mfaume ni tofauti na ile ya marehemu Ben Mtobwa. Na kama ni msomaji mzuri wa vitabu hata kama hujasoma gamba la nje la kitabu utagundua mwandishi ni nani. Hivyo haya mazoea yanaathiri sana filamu zetu.

"
PESA MBELE UBORA BAADAYE: wasanii wengi sasa wameweka pesa mbele huku wakimdharau mtanzania ambaye amekubali kuwa mtumwa wa kazi zao. Hawajali kuwa filamu ni mbovu ama inalandana na filamu ya fulani wanachoangalia ni mifukoni itaingia shilingi ngapi,hivyo hivyo kwa msambazaji ananunua filamu bila kuchukua wakati kuzipitia walau kidogo,matokeo yake anasambaza filamu ambayo miezi miwili iliyopita alisambaza pia.

"HAILLE SELLASIE"
UDHAIFU WA BODI YA FILAMU:  Bodi ya filamu Tanzania ni kama haipo vile,hiki ndicho chombo kikuu chenye madaraka ya kuuondoa huu uozo,lakini wamekuwa kimya sana na filamu zinaendelea kupeta licha ya kufanana fanana. Laiti kama filamu kadhaa zingefungiwa nadhani wengine wangeshtuka na kubadilika….mzani wa kupim filamu UNAHITAJIKA!!!!

"BEATRICE NYOROKA"
KUJILIMBIKIZIA MADARAKA: mwanzoni wakati msanii anaanza kuibukia unakuta anajitambulisha kama muigizaji lakini baada ya kupata jina kidogo tu utasikia oooh!! Mi mtunzi wa stori,mara naandika script kabla hatujakaa sawa mara anasema yeye director na pia ana idea ya kuedit hivyo muda si mrefu ataanza kuedit movie zake. Kwa mtindo huo wa kujifanya kujua kila kitu kweli atakawia kuiba filamu za nje na kutubadilishia lugha???.

"BOAZ KIM"
NATAKA KUWA KANUMBA: Katika mpira wa miguu ukimuuliza chipukizi ana ndoto gani atakujibu anataka kucheza ulaya lakini ukimuuliza msanii mchanga wa bongo ndoto yake ni ipi katika hii tasnia atakujibu “nataka kuwa kama kanumba” kwa ndoto hii sasa atajaribu kuigiza kama Kanumba na mwisho wa siku atatunga stori anazotunga Kanumba na hatimaye atatoa filamu kama ya Kanumba,sijui hapo ndo kutimiza ndoto ama kulivuruga soko la filamu. Si kwamba watu wasiwe na ndoto lakini zisiwe ndoto za kufananisha kazi. 




 












No comments:

Post a Comment