Monday, November 8, 2010

Utengenezaji wa filamu ya Binti Nusa 2





Katika kutengeneza filamu huwa kuna kuwa na hatua kadhaa, Pre-Production, Production, na Post-Production. Katika Pre-Production ndipo hufanyika kazi ya kutayarisha utengenezaji wa filamu, script huandikwa, wasanii hutafutwa, maeneo ambayo picha zitapigwa hutafutwa, kampuni ya kupiga picha hujulikana wakati huu na watendaji wote kwa ujumla , kila kitu kikisha kuwa tayari ndipo, hatua ya pili ya production huanza, ambapo ndio hufanywa kazi ya shooting ya filamu.
Kazi ya shooting ikishakamilika, huanza hatua ya Post Production, ambapo katika hatua hii ndo filamu huanza kufanyiwa kazi katika studio. Kuiedit, kuingiza sauti mbali mbali ili filamu iwe kamili, tayari kwa kusambazwa. BINTI NUSA 2 ipo katika hatua hii kaeni chonjo.

No comments:

Post a Comment